Stori: waandishi Wetu/Ijumaa
HOFU! Waigizaji wa tasnia ya filamu Tanzania, ambao walikuwa wameanza kusahausahau misiba mfululizo iliyowatokea miaka michache iliyopita, juzikati walijikuta wakitoneshwa kidonda, baada ya kutokea kifo cha muigizaji Tino Madhahabu, kilichotokea Tunduma mkoani Mbeya, kufuatia kuugua kwa muda mrefu.
HOFU! Waigizaji wa tasnia ya filamu Tanzania, ambao walikuwa wameanza kusahausahau misiba mfululizo iliyowatokea miaka michache iliyopita, juzikati walijikuta wakitoneshwa kidonda, baada ya kutokea kifo cha muigizaji Tino Madhahabu, kilichotokea Tunduma mkoani Mbeya, kufuatia kuugua kwa muda mrefu.
Kifo hicho kimeibua hofu upya kwa wasanii wa Bongo Muvi, hasa ikikumbukwa kuwa mchunguji mmoja (jina tunalihifadhi) aliwahi kutabiri kuwa, wimbi hilo la vifo litaendelea tena mwaka huu kwa wasanii na watu wengine maarufu, wakiwemo wanasiasa hivyo kuwataka kumrudia Mungu.
Wasanii kadhaa waliozungumza na Ijumaa
baada ya taarifa za msiba huo walionesha hofu ya kifo waliyonayo lakini
wengi wakasema Kifo cha Tino ni mipango ya Mungu hivyo kila mmoja
ajiandae tu.
Msanii aliyewahi kufanya kazi kwa karibu na Tino, Kulwa Kikumba ‘Dude’ alisema: “ Dah! Ni kweli jamaa katutoka, kikubwa tumuombee na hilo la hofu ni vyema kila mmoja akawa nayo ili aweze kujiandaa kwa safari.”
Msanii aliyewahi kufanya kazi kwa karibu na Tino, Kulwa Kikumba ‘Dude’ alisema: “ Dah! Ni kweli jamaa katutoka, kikubwa tumuombee na hilo la hofu ni vyema kila mmoja akawa nayo ili aweze kujiandaa kwa safari.”
Msanii wa filamu Bongo, Devota Mbaga.
Katika kuonesha kuweweseka, msanii mwingine wa filamu, Miriam Jolwa
‘Jini Kabula’ alisema: “Mimi sitakufa kwa kuwa niko karibu na Mungu,
watakaokufa ni wale walio mbali na Mungu.”Msanii mwingine, Isabela alisema kifo cha Tino kimemshtua mno na kusema ni mapenzi ya Mungu, lakini akaponda utabiri wa mchungaji akisema hajawahi kuamini mambo hayo, kauli ambayo pia ilitolewa na Rose
0 comments: